OFA!! OFA!! - PATA MSAADA KWA WATAALAMU WA IT BURE, TEMBELEA TUVUTI KWA KUBONYEZA HAPA AU WHATSAPP: +255678 920112
News
Loading...

BREAKING NEWS/HABARI ZA HIVI PUNDE PAGE 3


Hallo!! Breaking News za Leo Soma kwenye Ubao wetu Mweusi

BREAKING NEWS ZA TAREHE 05/05/2017

AJALI DAR:
Watu 2 wamekufa, 1 ajeruhiwa baada ya Fuso la nyanya kutoka Iringa kuligonga lori la Mchanga kwa nyuma eneo la Tabata Mwananchi, Polisi wathibitisha.'

MAAFA TANGA:
Watu 2 wafa, 8 wajeruhiwa baada ya kutokea mafuriko kijijini Magila, Kata ya Mkumbara, Korogwe, RPC Wakulyamba athibitisha. Tathmini inafanyika.'

AJALI ARUSHA:
Wanafunzi na Walimu wa shule ya Lucky Vincent ya Arusha wafariki baada ya gari lao kutumbukia Mto Malela wilayani Karatu. Taarifa zaidi zitafuata.'

AJALI KARATU:
Polisi wathibitisha kuwa watoto 31 na walimu wamefariki katika ajali iliyotokea katika Mto Malera.'

AJALI KARATU:
Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa RC wa Arusha Mrisho Ganbo kufuatia vifo vya wanafunzi 32, Walimu 2 na dereva wa shule ya Lucky Vicent.'


BREAKING NEWS ZA TAREHE 04/05/2017


JPM ATEUA:
Rais John Magufuli amemteua Prof Egid Beatus Mubofu kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania "TBS" Ikulu yasema .'


VIWANGO FIFA:
Tanzania yabaki nafasi ya 135 katika msimamo wa viwango vya FIFA uliotoka leo. Kenya yabaki 78 na Uganda 72. Brazil yaendelea kuongoza kwa ubora.'


MATUMIZI YA EFD:
Meneja msaidizi Viwanja vya Leaders Club, Emmanuel Chacha ashtakiwa kortini Kinondoni, Dar kwa makosa 2 ikiwemo kutotumia EFD kutolea risiti.'

KOCHA MPYA:
Kocha Stuart Baxter ataondoka Supersport United mwishoni mwa msimu na kujiunga na timu ya Taifa ya Afrika Kusini "Bafana Bafana",SAFA yatangaza leo.'

BENITEZ MATATANI:
Kocha wa Newcastle Rafael Benitez ashtakiwa na FA kwa kutoa maoni dhidi ya refa aliyechezesha mechi ya timu yake vs. Preston kabla ya pambano.'

VITI MAALUM:
Catherine Ruge ameteuliwa kuwa mbunge Viti Maalum kupitia Chadema, NEC yasema, Ruge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Dr Macha aliyefariki Machi 31.'



BREAKING NEWS ZA TAREHE 03/05/2017

UBUNGE EALA:
Kamati kuu Chadema yateua watu 6 kugombea nafasi 2 za ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Tumaini Makene atangaza. Maisha,Wenje, Prof Safari wamo .'

MAHOJIANO NA MAALIM:
Hakuna CUF-Lipumba wala CUF-Maalim bali maamuzi ya chama yanafanywa na Baraza Kuu, asema Maalim Seif katika mahojiano kituo cha Clauds TV.'

MAHOJIANO NA MAALIM:
Maalim Seif adai, kupitia Clauds TV, kuwa alijitoa kwenye mazungumzo na Rais Shein baada ya tarehe ya marudio ya uchaguzi kutangazwa.'

MAHOJIANO NA MAALIM:
Maalim Seif asema kamwe hawezi kuketi meza moja ya mazungumzo na Prof Lipumba kwa madai kuwa mwanasiasa huyo alikisaliti chama cha CUF.'

MKONO WA MAALIM:
Nilifanya maksudi kutompa mkono Rais Shein kwa ili apate ujumbe kuwa nilikasirika kuporwa haki yangu, asema Maalim Seif kupitia Clouds TV.'

FAINALI FA:
Mechi ya Fainali ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba na Mbao FC itachezwa katika Uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma, Rais wa TFF, Jamal Malinzi atangaza.'

AJALI DAR:
Watu 2 wafa, 15 wajeruhiwa baada ya daladala kugongana na lori jirani na duka Lifemate, Temeke, RPC Muroto asema. Miili yahifadhiwa hospitalini Temeke.'

PEMBA MBARONI:
Polisi wa Tz, Uganda wanamchunguza Mtanzania Jack Pemba aliyekamatiwa Entebe, nchini Uganda akituhumiwa kutakatisha fedha, Daily Monitor laripoti.'

VYETI FEKI:
Waziri Kairuki asema bungeni, wanaodai kuonewa wakate rufaa Utumishi, aonya adhabu zaidi kuwakabili wakishindwa kudhibitisha uhalali wa vyeti vyao.'

BAJETI:
Waziri Ummy aomba Bunge lipitishe Sh1.16trn za Bajeti ya Wizara ya Afya 2017/2018. Kamati yasema serikali haikutoa asilimia 50 ya fedha 2016/2017.'

UCHAGUZI KENYA:
Chama cha Jubilee chamtangaza mwanamuziki, Charles Njagua "Jaguar" mshindi mchujo wa kupata nafasi kuwania ubunge wa jimbo la Starehe, Nairobi.'


BREAKING NEWS ZA TAREHE 02/05/2017


MAJERAHA YA IBRA:
Straika wa Man United Zlatan Ibrahimovic amefanyiwa upasuaji wa goti wenye mafanikio, atarajiwa kupona mapema, wakala wake Mino Raiola asema.'

MDEE HATIANI:
Mbunge Halima Mdee akutwa na hatia ya kudharau mamlaka ya spika, kutoa lugha ya matusi, kamati yasema. Yataka azuiwe kuhudhuria vikao vilivyobaki.'

BULAYA HATIANI:
Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya ameitwa hatiani kwa kudharau mamlaka ya Spika, kamati ya Bunge yatangaza na kupendekeza na kupendekeza apewe karipio kali.'


MBOWE HATIANI:
Kiongozi Kambi Rasmi ya upinzani, Freeman Mbowe akutwa na hatia ya kudharau mamlaka ya spita,aomba radhi na kusamehewa, Kamati ya Maadili yasema.'

UAMUZI WA BUNGE:
Bunge lawasamehe Freeman Mbowe na DC Mnyeti bila masharti yoyote, Ester Bulaya kuandikiwa barua ya onyo huku Mdee akisamehewa kwa masharti.'


KAMATI YA BUNGE:
Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge yapendekeza DC Alexander Mnyeti asamehewe baada ya kuomba radhi kutokana na kosa la kulidharau Bunge.'

KESI YA WEMA:
Upelelezi wa kesi ya kukutwa na bangi inayomkabili Miss Tz 2006, Wema Sepetu wakamilika, Korti ya Kisutu yaelezwa. Kesi kuanza kusikiliz

http://ictyetu.blogspot.com/p/breakingnews-za-tarehe-28042017.html

0 Maoni :

Post a Comment