Leave a message
OFA!! OFA!! - PATA MSAADA KWA WATAALAMU WA IT BURE, TEMBELEA TUVUTI KWA KUBONYEZA HAPA AU WHATSAPP: +255678 920112
News
Loading...

WOMEN’S DAY: Je,Unafahamu kuwa wanawake wamevumbua vitu vingi katika Teknolojia? Soma hapa

Leo ni siku ya Wanawake Duniani, Mwanamke akijituma daima hufanya mambo makubwa sana kwa kuwa anaujasiri wa kutosha. Katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia kwa ujumla kuna wanawake wengi wameweza kugundua mambo ambayo ukiyasikia huwezi kuamini, Kwa mfano kwa mara ya kwanza nilipokuwa darasani nasoma Programming, nilihisi kuwa James Gosling ndiye aliyegundua mambo hayo, la hasha nilivyosoma na kugundua kuwa Ada lovelace ndiye mwanamama aliyekuwa wa kwanza katika programming, yaani ni programmer wa kwanza nilishangaa sana na tangu siku hiyo niliamini kuwa Mwanamke anaweza, ila ni muoga tu kudhubutu.


Leo March 8 2017 ni siku ya Wanawake Duniani hivyo sio vibaya kama tukicheki michango mbalimbali iliyofanywa na wanawake katika sekta muhimu ya sayansi na teknolojia ambapo mara nyingi hutawaliwa na wanaume. Nimekuletea list ya wanawake kumi waliyofanya uvumbuzi wa vitu mbalimbali ambavyo vilibadilisha historia ya teknolojia duniani.





1:Florence Parpart. Mwaka 1914 Florence Parpart alivumbua friji la kisasa linalotumia umeme ambapo uvumbuzi huo uliweka rekodi ya dunia hasa baada ya kuvumbuliwa na mwanamke.



2: Marie Van Brittan. Anajulikana zaidi kwa mchango wake mkubwa katika uvumbuzi wa kamera za CCTV mwaka 1969, ambapo ugunduzi huu aliufanya baada ya kukithiri kwa uhalifu katika jiji la Newyork.



3: Stephanie Kwole
k atakumbukwa kwa uvumbuzi wake wa material yaliyotumika kutengeneza bullet proof, vikoti ambavyo huvaliwa kwa ajili ya kuzuia risasi isiingie mwilini.



4: Hedy Lamarr: Ni mwafizikia aliyebobea katika maswala ya mawasiliano ambapo aligundua teknolojia ya wireless iliyosaidia kuanzishwa kwa wiFi na mfumo wa GPS.



5: Josephene Cochrane. Mwaka 1887 Josephene Cochrane alivumbua machine ya kuoshea vyombo au dish washer ambazo alikuwa akiziuza mahotelini mwaka mmoja baadae alifungua kiwanda chake.


http://ictyetu.blogspot.com/p/6letitia-gee.html

Shiriki(Share) kwenye Google Plus

About ICT yetu

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Maoni :

Post a Comment

a