OFA!! OFA!! - PATA MSAADA KWA WATAALAMU WA IT BURE, TEMBELEA TUVUTI KWA KUBONYEZA HAPA AU WHATSAPP: +255678 920112
News
Loading...

Usifanye vitu hivi kwenye simu yako ya SmartPhone! (Things you should never do on your SmartPhone)

Simu zetu ni muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku, kila mmoja anatumia simu yake kwa lengo tofauti tofauti, Lakini unapokwenda dukani kununua simu mpya je, ulishawahi kuuliza ni vitu gani sitakiwi kuvifanya kwenye hiyo simu? Kwa ushauri ni kwamba unapokuwa na wazo la kununua simu mpya cha kufanya kabla hujafika dukani anza ku revew/ kusoma maelezo kamili juu ya simu unayohitaji kununua, ili utambue je inakufaa au haikufai? Sihitaji kuongelea sana kuhusu hilo.

Twende kwenye somo letu la leo, Unaponunua simu yako basi tahadhari kuto kufanya vitu vifuatavyo:

1. Usitumie Public WiFi Networks



Habari yeyote unayoituma au kupokea kupitia public WiFi huwa inapatikana kwa mtu yeyote mwenye upeo wa kutafuta habari hiyo. Mfumo huo wa connection unatoa ruhusa kwa wezi wa mitandao yaani hackers kupekua habari zako kiurahisi, Sasa unapaswa kutumia WiFi network ambayo inalindwa na password nah ii itakusaidi wewe kulinda taarifa zako. (Mfano wa Public WiFi Network, Kwa Dar es salaam inapatikana Stendi kuu ya dala dala Ubungo,Mlimani City na sehemu zingine)

2. Usibonyeze Links hatari

Kuna baadhi ya wezi wa mitandao yaani hackers wanaweza kutma link Fulani kwenye email yako ili kutaka ku confirm na ukisha bonyeza hizo links tayari umewapa uwanja wa kutuma taarifa zako bila wewe kujua, Angalizo: usipende kubonyeza links za confirmation ambazo huzifahamu unaweza ukajuta mwisho wa siku.

3. Kutofunga Apps au programu baada ya kumaliza kutumia


Unapomaliza kutumia App yako usipende ku minimize badala ya kufunga kabisa. Wakati mwingine kwenye screen haionekani lakini kumbe kwa ndani bado ina run bila wewe kujua, athari yake ni kuisha kwa betri kwa haraka sana kuwa simu yako muda mwingi kuna App zinafanya kazi kwa ndani bila wewe kujua.

4. Kupost kwa marafiki sehemu ulipo au kufungua Location kwenye simu yako


Unaweza ukawa kwenye sherehe Fulani, ili marafiki zako kuwajulisha unaweza ukapost kuwa upo wapi na una marafiki wangapi mna sherehekea hiyo part. Na wakati mwingine unaweza ukaamua kuacha wazi mfano Google Location yaani GPS una turn on, hapo si kwamba unaruhusu marafiki wazuri tu wakufahamu mahali ulipo bali unarukhusu pia maadui wakupate kiurahisi, hivyo basi ni mbaya sana kuweka location wazi kwa wakati wote unaweza ukawa kwenye mazingira hatarishi.

5. Kutumia Chaja ya bei nafuu


Unapotumia chaja ya gharama nafuu unaweza ukaharibu simu yako, tumia chaja ambazo zenye nembo ya kampuni na zenye ubora.

6. Usitumie Simu yako wakati upo chooni


Dr Ron Cutler, director of biomedical science degrees at Queen Mary’s University London,alisema kwamba unapotumia simu yako wakati upo chooni unaruhusu baadhi ya bacteria kuvutika kwenye mikono yako uliyoshika simu

8. Kujibu meseji ambazo hujui zilipotoka

Kama unapata ujumbe wa meseji ambao hufahamu wapi umetoka, yapaswa anza kuuliza kwanza yeye ni nani kabla hujaanza kujibu ujumbe huo. Unaweza ukajiingiza kwenye hatari unapojibu kitu ambacho hujui kinamaana gani na wapi kimetoka.

9. Epuka au Skip Security software

10. Usi update Software mara kwa mara
Shiriki(Share) kwenye Google Plus

About ICT yetu

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Maoni :

Post a Comment