OFA!! OFA!! - PATA MSAADA KWA WATAALAMU WA IT BURE, TEMBELEA TUVUTI KWA KUBONYEZA HAPA AU WHATSAPP: +255678 920112
News
Loading...

Fahamu jinsi ya kuandika meseji zitakazojituma zenyewe baadae

Siku hizi maisha yanakimbia sana na kila kukicha majukumu yanaongezeka kwa kasi ya ajabu, ni rahisi sana kusahau baadhi ya ratiba kama kufanya mawasiliano na watu wako wa muhimu. Hapa ndipo umuhimu wa kuwa na uwezo wa kuset meseji zinazojituma unapokuja.



Simu nyingi za kisasa zina uwezo huu wa kutuma kuandaa sms ambazo zitajituma baadae maarufu kama Scheduled sms, ila kwa leo tutaangalia jinsi ya kuset scheduled sms katika simu za tecno zinazotumia mfumo wa HiOS.


Njia za kufuata;


1. Nenda kwenye message katika simu yako ya android

2. Nenda kwenye thread (ujumbe) wa mtu ambaye unataka kuwasiliana naye au fungua sehemu ya kuandika sms mpya, kisha chagua mtu unayetaka kumtumia. Alafu bonyeza kitufe cha utility (kipo na alama ya jumlisha chini kabisa katika sehemu ya kuandika sms).

3. Baada ya hapo swipe kwenda kushoto na utaona sehemu iliyoandikwa scheduled sms, baada ya kubonyeza hapo kuna ukurasa utatokea ambao utakuwezesha kuset muda na tarehe ambayo utapenda hiyo sms itumwe. Kumbuka unatakiwa uset dakika sita mbele au zaidi ya muda unaoandaa hiyo sms. Kisha bonyeza done.

4. Baada ya hapo unaweza ukaandika sms yako, na utaona kuna kama alama ya saa pembezoni mwa hiyo sms ikimaanisha kuwa hiyo sms inasubiri muda wake ufike ili itumwe.


Pakua App hii kwenye Play store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=dtd.phs.sil&hl=en







Tazama Video kwa mafunzo zaidi:




Shiriki(Share) kwenye Google Plus

About ICT yetu

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Maoni :

Post a Comment